

Lugha Nyingine
Uganda, DRC zakubaliana kufanya doria za pamoja katika Ziwa Edward kufuatia shambulizi kubwa
Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) zimekubaliana kuimarisha operesheni za pamoja za kiusalama kwenye eneo la Ziwa Edward baada ya kutokea kwa shambulizi kubwa lililofanywa na watu wanaodhaniwa kuwa wapiganaji wa Kongo.
Msemaji wa Jeshi la Uganda (UPDF) Kiconco Tabaro amesema kwenye taarifa iliyotolewa Jumatano wiki hii kuwa makamanda wa UPDF na Jeshi la DRC (FARDC) wamekutana katika Bandari ya Kasindi katika eneo la Beni la DRC, kwa nia ya kuimarisha uratibu wa jeshi la majini na mifumo ya usalama kando ya Ziwa Edward.
Aidha, wamekubaliana kuchukua hatua za kuhimiza ushirikiano ikiwemo kufanya doria za pamoja kwenye Ziwa hilo, kufanya mikutano ya uratibu wa mambo ya usalama na uvuvi kila baada ya muda, na kuelimisha jamii ya wavuvi.
Misri yafunga Jumba la Makumbusho Kuu la Misri kwa ajili ya kufunguliwa rasmi
Mwezi mpevu wavutia kote China wakati wa Sikukuu ya Mbalamwezi ya China
Wanasarakasi wafanya maonyesho katika Eneo la Ulimwengu wa Sarakasi la Wuqiao mjini Cangzhou, China
Sikukuu ya mavuno ya wakulima yaadhimishwa katika Mkoa wa Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma