Asilimia 86 ya wahojiwa duniani wasifu maendeleo ya China katika teknoloji ya kidijitali

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Mei 08, 2025

Roboti ikionekana katika picha kwenye Mkutano wa 8 wa Kilele wa China ya Kidigitali mjini Fuzhou, Mkoa wa Fujian, kusini mashariki mwa China, Aprili 29, 2025. (Xinhua/Lin Shanchuan)

Roboti ikionekana katika picha kwenye Mkutano wa 8 wa Kilele wa China ya Kidigitali mjini Fuzhou, Mkoa wa Fujian, kusini mashariki mwa China, Aprili 29, 2025. (Xinhua/Lin Shanchuan)

BEIJING - Ripoti ya Mtazamo wa Umma kwa Teknolojia ya Kidijitali Mwaka 2025 iliyotolewa Beijing Jumatano na Chuo Kikuu cha Renmin cha China imesema, asilimia 86 ya wahojiwa duniani kwenye utafiti wamesifu maendeleo ya China katika teknolojia ya kidijitali.

Utafiti huo uliofanywa na Kituo cha Utafiti wa Maoni Duniani cha chuo hicho, umewafanyia hojaji washiriki 7,599 kutoka nchi 38 kupitia sampuli ya kimataifa ya mtandaoni.

Ripoti hiyo imehusisha maeneo matano muhimu, yakiwemo maboresho katika maisha ya kila siku yanayoletwa na teknolojia ya kidijitali, matarajio na wasiwasi kuhusu teknolojia ya AI, na kuongezeka kwa utambuzi wa teknolojia ya kidijitali ya China katika Nchi za Kusini.

Uchambuzi wa data wa kikanda unaonyesha viwango vya juu zaidi vya kukubalika kwa teknolojia ya kidijitali ya China -- Afrika kwa asilimia 94.3, Amerika Kusini kwa asilimia 93, Asia Kusini-Mashariki kwa asilimia 91.1, Asia Kusini na Asia ya Kati asilimia 90.7, na Mashariki ya Kati asilimia 88.1.

Ripoti hiyo inasema, zaidi ya nusu ya wahojiwa wanaona teknolojia ya AI na biashara ya mtandaoni ni sekta zinazoongoza za kidijitali nchini China, ambapo majukwaa ya biashara ya mtandaoni kama Temu na SHEIN yamekua kwa kasi duniani kote kupitia nguvu ya ushindani wa bei na minyororo yenye ufanisi wa usambazaji bidhaa.

Wakati huo huo, utafiti huo umeonesha kuwa kampuni za AI za China zinasonga mbele haraka kwa mikakati ya maendeleo ya ufunguaji mlango na ya haraka, na katika maeneo kama vile Afrika, AI ya China inazidi kuchukuliwa kuwa kichocheo cha miundombinu ya kisasa na usimamizi wa kidijitali, ripoti hiyo imesema.

"Kampuni za teknolojia za China zinaonekana sana kuwa vinara katika uvumbuzi wa kidijitali. Mapema mwaka huu, muundo wa R1 wa DeepSeek ulitoa ufanisi thabiti kwa kutumia rasilimali chache za kompyuta. Mifumo mikubwa ya lugha ya Tencent ya Hunyuan na Qwen ya Alibaba pia imechukua nafasi za mbele zenye ufanisi katika upimaji na majaribio ya kimsingi. Wakati huo huo, Alipay na WeChat Pay zinaendelea kupanuka duniani kote,” Zhang profesa wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano katika chuo kikuu hicho amesema.

Ripoti hiyo pia inasema kuwa asilimia 83.6 ya wahojiwa wa Nchi za Kusini South wanaona teknolojia ya kidijitali ya China kuwa nguvu yenye uhasama katika nchi zao. Inaeleza kuwa, ushirikiano katika teknolojia, miundombinu, na ukuzaji wa vipaji unaimarika, ukiunga mkono utandawazi wa kampuni za kiteknolojia za China na ukuaji wa kidijitali katika nchi hizo.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha